Posts

Showing posts from March, 2026

KASRI 2

Image
"Hapana Albert, ukiondoka kila kitu kitajulikana......naweza kunyongwa kwa kosa la kumdanganya mfalme kwa miaka yote hiyo....." Helena alisimama akimsihi Albert asiondoke huku akiwa ameushika mkono wake..... Kimya kilitawala kidogo ambapo Albert na Helena walisikia kama nguo ikikwaruza ukuta, ilikuwa ni kama mtu aliyejibanza na ukuta akijaribu kusogea mbali baada ya kusikiliza mazungumzo yale. Albert alizunguka nyuma ya ukuta ule kulipokuwa na chumba cha stoo kisha akamdaka mtu aliyekuwa kwenye harakati za kunyata ili aondoke eneo lile. “ Tulia hapo, we ni nani....".Albert alimuuliza na kabla hajapewa jibu alimtambua mtu yule kwamba ni James, mtoto wa mke wa kwanza wa mfalme. Albert aliuachia mkono wa James huku akishangaa kwa hofu akijua kwamba siri kubwa imejulikana... “ Wewe umefata nini hapa, umesikia kitu gani.. " James bila kuzungumza chochote aliondoka akimkata Albert jicho kali. Albert aligeuka na kumfuata Helen ambaye kwa wakati huo alikuwa amejibanza ukut...

Small rituals, lasting love

Image
In a small town, an elderly man used to visit the same tea shop every morning. He always sat in the corner, ordered one cup of tea, and quietly watched the street. The shop owner noticed something unusual. Every day, the man would take a small piece of bread from his pocket and crumble it on the windowsill. Within minutes, a few stray cats would gather outside, waiting patiently. The man never rushed them. He would just smile softly, sip his tea, and feed them. One rainy morning, the man didn’t come. The shop owner felt something was missing. The corner felt emptier than usual. But then something surprising happened, the cats still came. They gathered at the same window, looking inside, as if waiting. The next day, the owner brought bread and placed it on the windowsill. The cats ate quietly. From that day on, the shop owner continued the small ritual. No big speeches, no dramatic changes; just tea, bread, and quiet kindness. Over time, more people noticed. Some began leaving food too....

K A S R I

Image
Mfalme Duncan alikuwa akipigana vita kwa takribani miezi sita kwa ajili ya kulinda jiji la Haven. Jiji hili lilikuwa na watu wengi, uongozi wake ulikuwa imara na jeshi lisilopigwa na maadui zake. Wakazi wengi ambao ni wazaliwa na wahamiaji kutoka vijiji jirani, hujishughulisha na shughuli mbalimbali. Ni kijiji tajiri kwa madini na kilimo. Hata hivyo, kutokana na utajiri wa wananchi wake, watoto huzaliwa wakiishi katika mazingira mazuri. Wazee huozesha binti zao kwa kupokea mahari za dhahabu na Vito vingi vya thamani. Hata hivyo, sio rahisi kuingia katika himaya hii ya kifalme yenye sheria kali.  Baada ya kutoka vitani Mfalme aliwaita wake zake watatu; Charlotte , Helena na Victoria pamoja na watoto wake wote ; Elsa, James, Albert, Rose na Belle. Charlotte, aliyevaa gauni refu, la njano, ni mke wa kwanza wa Mfalme Duncan, ana watumishi wapatao mia moja kwa ajili ya kumuhudumia kwa kila atakachohitaji. Charlotte ni mpiganaji vita, aliolewa baada ya baba yake kushindwa vita na Mfalme...